Na Mwandishi Wetu
TIMU ya
Soka ya Uswahilini FC imeibuka mabingwa wa Kombe la Mama Shija baada ya
kuichapa Wamangati zote za Mbagala katika fainali ilijaa ushindani
mkubwa iliyofanyika uwanja wa Shule ya Msingi Kingunge, Mbagala Dar es
Salaam.
Katika fainali hizo ambazo zilidhaminiwa na Kampuni
ya Simu ya Vodacoma, mshambuliaji Sultani Kasikasi wa Uswahilini
aliibuka mchezaji bora wa mchezo huo baada ya kuifungia timu yake mabao 3
yaliyoipatia timu yake ubingwa na kuzawadiwa mpira "hat Trick".
Mabao
ya Kasikasi yalipatikana dakika ya 32 , dakika ya 41 na 59 na mabao ya
WAmangati yaliyungwa na Salum Gava dakika ya 39 na bao la pili
lilifungwa na Musa Madebe aliyeunganisha krosi safi ya Shaaban Pazi.
Muandaaji
wa mashindano hayo, Fatuma Shija akizipongeza timu zote 20
zilizoshiriki Kombe hilo aliwataka vijana kutumia muda wao mwingi kwenye
michezo ambayo itachukua muda wao mwingi kujenga miili yao badala ya
kuvuta bangi na kufanya vitendo vya kihuni mitaani.
Mashindano
hayo yalishirikisha timu kuoka Mkuranga mkoa wa Pwani, Wilaya Mpya ya
Kigamboni na Temeke, Mshindi wa nne ilikuwa timu ya Kisemvule FC
iliyezawadiwa mpira mmoja, mshindi wa tatu ni Bodabdoda iliyopata jezi
seti moja na mpira mmoja na mshindi wa pili alipata medali 15 za shaba,
jezi seti mbili na mpira mmoja.
Ilikuwa furaha kubwa
kwa mashabiki wa Uswahili baada ya kuzawadiwa Kombe na medali 15 za
dhahabu kwa wachezaji wake, jezi seti mbili na mpira mmoja walishangilia
na kucheza uwanja mzima huku kuimba nyimbo za ushindi na kuwavutia
mashabiki wake na wapita njia.
mwisho
.
No comments:
Post a Comment