MWENDA BLOG
Friday, May 24, 2013
TAIFA STARS MCHANA WAITWA IKULU KUTETA NA RAIS
Taarifa ambazo Lenzi ya Michezo imezipata zinasema Taifa stars imeitwa na Rais leo mchana kula chakula cha mchana paamoja na mambo mengine ambayo yatafahamika baadae.
Stars asubuhi imefanya mazoezi kwenye uwanja wa Karume ikiwa na wachezaji 21 kwani Mwinyi Kazimoto aliumia mguu na Salum Abubakar amefiwa na baba yake mlezi hivyo amekwenda kuhudhuria msiba huo
NZERA KITANO REDD'S MISS KIBAHA 2013
Katikati Redds Miss Kibaha Nzera Kitano , kushoto
mshindi wa pili Ester Albert na kulia ni Rachel Joh ambaye ni mshindi wa tatu.
Na Ripota Wetu, Kibaha
ALIYEKUWA mshiriki namba 6
katika shindano la kumsaka Redds Miss Kibaha 2013 Nzera Kitano ameibuka kua Redds Miss Kibaha 2013
katika shindano lililofanyika kwenye ukumbi wa Conteainer Kibaha Maili Moja mkoani Pwani Mei 17 mwaka
huu
Nzera ambae alionekana kuwa
mchezi tangu mwanzo wa shindano aliweza kupenya katika hatua ya nusu fainali
ambapo aliingia katika warembo watano bora kati ya washiriki 10 waliokuwa
wakishindana kuwania taji hilo.
Aidha kwa ushindi huo Nzera amepata zawadi ya fedha taslimu
sh.300,000 pia amepa ofa ya kwenda kuchagua vipodozi na mapambo ya aina
mbalimbali katika duka la Shear Illusion lilipo Mlimani City pamoja na
king’amuzi kutoka kampuni ya Multichoice ambapo atafungiwa bure.
Mshindi wa pili ni Ester
Albert ambaye amepata fedha taslimu kiasi cha sh.200,000 pia atapata ofa ya
kulipiwa ada ya shule au kutafutiwa kazi na mdau ambaye hataki kutaja kwenye
vyombo vya habari.
Mshindi wa tatu ni Rachel
John aliyepata fedha taslimu sh. 150,000 huku nafasi ya nne ikienda kwa Sylvia
John huku nafasi ya tano ilikwenda kwa Beatrice Bahaya.
Kwa ushindi huo warembo wote
watano wamepata nafasi ya kwenda kushiriki kwenye shindano la Redds Miss Pwani
watakakochuana na warembo wa Bagamoyo kuwania tiketi ya kwenda kushiriki katika
shindano la Kanda ikiwa ni katika kuwania tiketi ya shindano la taifa.
Shindano hilo limeandaliwa na
Kampuni ya Linda Media Solution (LIMSO) na kudhaminiwa na
Redds Miss Kibaha
ilidhaminiwa na Tanzania Distilleries Konyagi kupitia kinywaji cha Dododma
Wine, Redds Premium Cold, Fredito Entertainment, CXC Africa, Michuzi Media
Group |(MMG), Aco Catering & Servises, Pr Studio, ASET ,Santorine Holiday
Resort na Amazon Night Club.
Bendi ya Muziki wa dansi ya
Mashujaa ilitumbuiza na kuwachengua mashabi wa urembo wa mkoa wa Pwani.
CHEKI MCHUMBA WA NEY WA MITEGO A.K.A MAMA KIJACHO ALIVYO MREMBO AKIWA PENY WA DIAMOND PLATNUM DAR LIVE
| Diamond akisukuma kichwa cha Ney na mchumba wake ili wabusiane |
RAIS KIKWETE ATHIBITISHIA UMMA KWAMBA PSPF IKO IMARA NA HAITAKUFA
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.
Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Ndugu. Adam H. Mayingu tuzo ya kuwa Mfuko wa kwanza wa Hifadhi ya
Jamii Tanzania kutoa mikopo ya nyumba kwa wanachama wake. Tuzo hiyo ilitolewa kwenye maadhimisho ya
kilele cha Wiki ya Mifuko ya Jamii mjini Dodoma. Mh. Raisi alisema PSPF ni mfuko madhubuti na
una fursa nyingi za kimaendeleo kwa wananchi wa Tanzaniai na unauwezo mkubwa na
salama katika uwekezaji . Aliongezea kwa
kusema sio kweli kwamba Mfuko huu uko mahututi kama ilivyozungumziwa kwenye
baadhi ya vyombo vya habari, bali Mfuko huu unadai wadai wake Trilioni 6 na
kudai sio kufilisika tena
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa
Pensheni wa PSPF ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr.
Rehema J. Nchimbi kuhusu shughuli za Mfuko na fursa zilizopo kwa watanzania
hususani mikopo ya nyumba na mafao ya aina mbalimbali ikiwemo fao la
Ujasiliamali na Elimu.
BFT YAOMBA WADHAMINI
Na
Elizabeth John
KOCHA wa
timu ya taifa ya ngumi, Remmy Ngabo, ameitaka serikali na wadau wa ngumi nchini,
kujitolea kudhamini kambi ya mabondia 16 ambao
wanajiandaa na mashindano ya Majiji yanayotarajia kufanyika Julai 1 hadi 7
mwaka huu, jijini Mwanza.
Awali mashindano hayo yalipangwa kufanyika Juni 20 hadi 25,
kutokana na kutokuwa na maandalizi ya kutosha, wamelazimika kusogeza mbele
tarehe ya kufanyika kwa mashindano hayo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, alisema mabondia hao
kwasasa wanaendelea na mazoezi ya kujifua katika uwanja wa Taifa wa Ndani
jijini Dar es Salaam kwaajili ya maandalizi ya michuano hiyo.
“Mabondia wapo katika hali ngumu ya maandalizi hivyo wadau wa
mchezo huu tunawaomba wajitokeza kudhamini maandalizi haya,” alisema.
Alisema mashindano hayo ya Majiji ni maandaliazi ya kuwaweka sawa
mabondia kwaajili ya mashindano ya Afrika na Olimpiki ambayo yanatarajia
kufanyika hivi karibuni yakishirikisha mataifa mbalimbali.
Afande Sele kuachia albamu ya ‘Amani na Upendo’
Na Elizabeth John
MKONGWE wa muziki wa kizazi kipya
nchini ambaye anauwakilisha mkoa wa Morogoro, Seleman Msindi ‘Afande Sele’
ameachia albamu yake mpya inayojulikana kwa jina la ‘Amani na Upendo’.
Akizungumza na Habari Mseto jijini
Dar es Salaam, alisema licha ya soko la mauzo ya albamu kusuasua hatojali
mauzo mabaya kwakuwa lengo lake ni kuelimisha jamii na sio kupata maslahi.
“Sitofikilia soko kama litalipa au
vipi ninachohitaji ni kuwapa elimu watanzania, mashabiki wategemee kununua
albamu hiyo kwa bei rahisi,” alisema.
Alisema anaomba mashabiki waipokee
vizuri kazi hiyo na kwamba ina jumla ya nyimbo 10 ambazo zote zimefanya vizuri
katika soko hilo.
Afande sele alizitaja baadhi ya
nyimbo ambazo zipo katika albamu hiyo kuwa ni Kingdom, Karibu Morogoro, Karata
Dume na nyinginezo ambazo zinafanya vizuri katika soko hilo.
Subscribe to:
Posts (Atom)



