I made this widget at MyFlashFetish.com.

wise 1

hii

Friday, May 24, 2013

SPLASH WAJA NA IDENTTTY CARD







TAIFA STARS MCHANA WAITWA IKULU KUTETA NA RAIS



TIMU ya Taifa 'Taifa stars" ambayo ipo kambini kujiandaa na mchezo wa marudiano na Morocco wa kutafuta kufuzu fainali za dunia 2014 nchini Brazil imealikwa Ikulu kula chakula cha mchana leo.

Taarifa ambazo Lenzi ya Michezo imezipata zinasema Taifa stars imeitwa na Rais leo mchana kula chakula cha mchana paamoja na mambo mengine ambayo yatafahamika baadae.

Stars asubuhi imefanya mazoezi kwenye uwanja wa Karume ikiwa na wachezaji 21 kwani Mwinyi Kazimoto aliumia mguu na Salum Abubakar amefiwa na baba yake mlezi hivyo amekwenda kuhudhuria msiba huo


NZERA KITANO REDD'S MISS KIBAHA 2013




Katikati  Redds Miss Kibaha Nzera Kitano , kushoto mshindi wa pili Ester Albert na kulia ni Rachel Joh ambaye ni mshindi wa tatu.
Na Ripota Wetu, Kibaha
ALIYEKUWA mshiriki namba 6 katika shindano la kumsaka Redds Miss Kibaha 2013 Nzera  Kitano ameibuka kua Redds Miss Kibaha 2013 katika shindano lililofanyika kwenye ukumbi wa Conteainer  Kibaha Maili Moja mkoani Pwani Mei 17 mwaka huu
Nzera ambae alionekana kuwa mchezi tangu mwanzo wa shindano aliweza kupenya katika hatua ya nusu fainali ambapo aliingia katika warembo watano bora kati ya washiriki 10 waliokuwa wakishindana kuwania taji hilo.

 Aidha kwa ushindi huo  Nzera amepata zawadi ya fedha taslimu sh.300,000 pia amepa ofa ya kwenda kuchagua vipodozi na mapambo ya aina mbalimbali katika duka la Shear Illusion lilipo Mlimani City pamoja na king’amuzi kutoka kampuni ya Multichoice ambapo atafungiwa bure.
 
Mshindi wa pili ni Ester Albert ambaye amepata fedha taslimu kiasi cha sh.200,000 pia atapata ofa ya kulipiwa ada ya shule au kutafutiwa kazi na mdau ambaye hataki kutaja kwenye vyombo vya habari.
 
Mshindi wa tatu ni Rachel John aliyepata fedha taslimu sh. 150,000 huku nafasi ya nne ikienda kwa Sylvia John huku nafasi ya tano ilikwenda kwa Beatrice Bahaya.
 
Kwa ushindi huo warembo wote watano wamepata nafasi ya kwenda kushiriki kwenye shindano la Redds Miss Pwani watakakochuana na warembo wa Bagamoyo kuwania tiketi ya kwenda kushiriki katika shindano la Kanda ikiwa ni katika kuwania  tiketi ya shindano la taifa.
Shindano hilo limeandaliwa na Kampuni ya Linda Media Solution (LIMSO) na kudhaminiwa na
Redds Miss Kibaha ilidhaminiwa na Tanzania Distilleries Konyagi kupitia kinywaji cha Dododma Wine, Redds Premium Cold, Fredito Entertainment, CXC Africa, Michuzi Media Group |(MMG), Aco Catering & Servises, Pr Studio, ASET ,Santorine Holiday Resort na Amazon Night Club.
Bendi ya Muziki wa dansi ya Mashujaa ilitumbuiza na kuwachengua mashabi wa urembo wa mkoa wa Pwani.

CHEKI MCHUMBA WA NEY WA MITEGO A.K.A MAMA KIJACHO ALIVYO MREMBO AKIWA PENY WA DIAMOND PLATNUM DAR LIVE




clip_image001[16]
clip_image001
Bila shaka unafahamu kuwa Nay wa Mitego ni baba mtarajiwa. Mara nyingi Nay amekuwa akiweka picha ya mpenzi wake anayetarajia kumzalia mtoto hivi karibuni lakini hujawahi kuona picha yake inayoonekana vizuri zaidi. Tazama picha hizi za shemeji/wifi yetu zilizochukuliwa kwenye show ya Nay na Diamond, Dar Live weekend iliyopita.
clip_image001[6]
Diamond akisukuma kichwa cha Ney na mchumba wake ili wabusiane
clip_image001[8]
clip_image001[10]

RAIS KIKWETE ATHIBITISHIA UMMA KWAMBA PSPF IKO IMARA NA HAITAKUFA


 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Ndugu. Adam H. Mayingu  tuzo ya kuwa Mfuko wa kwanza wa Hifadhi ya Jamii Tanzania kutoa mikopo ya nyumba kwa wanachama wake.  Tuzo hiyo ilitolewa kwenye maadhimisho ya kilele cha Wiki ya Mifuko ya Jamii mjini Dodoma.  Mh. Raisi alisema PSPF ni mfuko madhubuti na una fursa nyingi za kimaendeleo kwa wananchi wa Tanzaniai na unauwezo mkubwa na salama katika uwekezaji .  Aliongezea kwa kusema sio kweli kwamba Mfuko huu uko mahututi kama ilivyozungumziwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari, bali Mfuko huu unadai wadai wake Trilioni 6 na kudai sio kufilisika tena

 Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete akisoma kipeperushi cha nyumba za PSPF zinazokopeshwa kwa wanachama wa Mfuko huo, huku akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa  Mfuko huo ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea kuhusu nyumba hizo na fursa zingine zilizopo PSPF kwa Watanzania ikiwa ni pamoja na ujumbe kwa Watanzania kwamba mtu yeyote mwenye umri usiopungua miaka 18 anaweza kuwa mwanachama wa PSPF

  Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF ndugu Adam H. Mayingu akimuelezea Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Rehema J. Nchimbi kuhusu shughuli za Mfuko na fursa zilizopo kwa watanzania hususani mikopo ya nyumba na mafao ya aina mbalimbali ikiwemo fao la Ujasiliamali na Elimu.
   Mtangazaji wa TBC Amina Mollel akikabidhi fomu ya kujiunga na PSPF kwa Meneja Masoko wa Mfuko huo Bi. Costantina Martin mala baada ya kuvutiwa na kukata shauri ya kuwa mwanachama wa Mfuko wa kwa njia ya uchangiaji wa hiari
Timu ya PSPF iliyokuwa kwenye maonyesho ya wiki ya hifadhi ya Jamii wakiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wao ndugu Adamu Mayingu katikati.  Timu hiyo inastahili pongezi kutokana na uduma bora waliyokuwa wakiitoa kwa wananchi waliokuwa wakitembelea banda hilo la PSPF pale Nyerere squire Dodoma.
Wanachama wa PSPF wakipata taarifa mbalimbali ikiwapo historia ya michango yao na taarifa za uanachama.

BFT YAOMBA WADHAMINI



Na Elizabeth John


KOCHA wa timu ya taifa ya ngumi, Remmy Ngabo, ameitaka serikali na wadau wa ngumi nchini, kujitolea kudhamini kambi ya mabondia 16 ambao wanajiandaa na mashindano ya Majiji yanayotarajia kufanyika Julai 1 hadi 7 mwaka huu, jijini Mwanza.
Awali mashindano hayo yalipangwa kufanyika Juni 20 hadi 25, kutokana na kutokuwa na maandalizi ya kutosha, wamelazimika kusogeza mbele tarehe ya kufanyika kwa mashindano hayo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, alisema mabondia hao kwasasa wanaendelea na mazoezi ya kujifua katika uwanja wa Taifa wa Ndani jijini Dar es Salaam kwaajili ya maandalizi ya michuano hiyo.
“Mabondia wapo katika hali ngumu ya maandalizi hivyo wadau wa mchezo huu tunawaomba wajitokeza kudhamini maandalizi haya,” alisema.
Alisema mashindano hayo ya Majiji ni maandaliazi ya kuwaweka sawa mabondia kwaajili ya mashindano ya Afrika na Olimpiki ambayo yanatarajia kufanyika hivi karibuni yakishirikisha mataifa mbalimbali.
“Maandalizi mazuri ya mashindano makubwa ni haya mashindano madogo, mabondia wanatakiwa kufanya mazoezi ya kutosha ili kushiriki mashindano hayo,” alisema Kocha huyo ambaye anatambulika na Shirikisho la Ngumi Duniani (AIBA).

Afande Sele kuachia albamu ya ‘Amani na Upendo’



Na Elizabeth John

MKONGWE wa muziki wa kizazi kipya nchini ambaye anauwakilisha mkoa wa Morogoro, Seleman Msindi ‘Afande Sele’ ameachia albamu yake mpya inayojulikana kwa jina la ‘Amani na Upendo’.

Akizungumza na Habari Mseto jijini Dar es Salaam, alisema licha ya soko la mauzo ya albamu kusuasua hatojali mauzo mabaya kwakuwa lengo lake ni kuelimisha jamii na sio kupata maslahi.

“Sitofikilia soko kama litalipa au vipi ninachohitaji ni kuwapa elimu watanzania, mashabiki wategemee kununua albamu hiyo kwa bei rahisi,” alisema.

Alisema anaomba mashabiki waipokee vizuri kazi hiyo na kwamba ina jumla ya nyimbo 10 ambazo zote zimefanya vizuri katika soko hilo.

Afande sele alizitaja baadhi ya nyimbo ambazo zipo katika albamu hiyo kuwa ni Kingdom, Karibu Morogoro, Karata Dume na nyinginezo ambazo zinafanya vizuri katika soko hilo.