TANGAZO ISERESPORTS COLLECTION

TANGAZO SHIWATA

Tuesday 22 September 2015

Isere Sports yapata tuzo ya UMITASHUMTA

Na Mwandishi Wetu

WADAU wa Michezo mkoa wa Dar es Salaam wametakiwa kujitokeza kuisaidia Serikali kukuza michezo na kufufua vipaji vya wachezaji katika fani mbalimbali katika shule za msingi na Sekondari.

Akizungumza katika sherehe ya kuwapongeza wachezaji na wadau mbalimbali walioshiriki michezo ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) Dar es Salaam juzi,Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mushi aliwataka wadau wa michezo kusaidia Serikali kufufua vipaji vya wachezaji.

Katika sherehe hizo ambazo mkoa wa mkoa wa Dar es Salaam waliotwaa ubingwa wa jumla za mashindano hayo yaliyofanyika mkoa wa Mwanza mwaka huu,Meneja wa timu ya UMITASHUMTA ya Mkoa wa Dar es Salaam, Adolf Ally alisema mikoa mingi ilidhamiria kupata ushindi huo lakii wao walijiandaa zaidi.

Mmoja wa wadau waliopata tuzo hiyo Kampuni ya Isere Sports, Abbas Ally ambao ni wauzaji wa vifaa michezo nchini aliahidi kuongeza vifaa vyenye ubora kwa bei nafuu ili mwakani mkoa huo uendelee kuwa mabingwa.

Mkoa wa Dar es Salaam uliochukua ushindi wa jumla kwa kutwaa medali  26 katika michezo mbalimbali lakini ikiwemo soka ya wanawake lakini ilijikuta inafungwa katika mchezo wa soka ya wamaume baada ya kupachikwa bao 1-0 na wenyeji Mwanza.

mwisho


No comments:

Post a Comment