TANGAZO ISERESPORTS COLLECTION

TANGAZO SHIWATA

Sunday, 27 January 2013

Njaa yapiga hodi Kondoa

Na Massare Damiani,Kondoa.
SHULE za msingi katika kata ya Hondomairo tarafa ya Kolo wilayani Kondoa huenda zikafungwa wakati wowote kutokana na kukosa chakula unaosababisha njaa kali ambapo wananchi sasa wanafikiria kuhama makazi yao kwenda maeneo mengine kuhemea chakula.

Kwa mujibu wa Diwani wa Kata ya Hondomairo, Bw. Kirangi Shaabani Hussein wakati akiwa njiani kuelekea ofisi za  halmashauri ya wilaya ya Kondoa kushughulikia tatizo hilo,alisema kuwa hali katika kata yake ni mbaya na kinachosikitisha zaidi ni kata yake kutokuwepo kwenye orodha ya mgao wa chakula tani 50 zilizotoloewa na serikali kuu.

Diwani Kirangi amelalamika kuwa kutokana na hali ngumu ya maisha hivi sasa katika kata yake wananchi kukosa chakula, hata shughuli za maendeleo zimekwama na wananchi wanashindwa kufanya kazi zao za mashambani kutokana na ulegevu walio nao.

"Nimekuwa nikitoa taarifa tangu mwaka jana Juni na serikali na halmashauri wamekuwa wakinisikia na kuahidi kushughulikia tatizo hilo,sasa inakuwaje leo kata yangu inakuwa haipo kwenye orodha ya mgawo wa chakula?amehoji diwani Kirangi kwa uchungu.

Alisema kuwa yeye mwenyewe amelazimika kutoa chakula alichokuwa nacho ndani ya nyumba yake magunia 10 na kuwagawia wananchi  akidhani kuwa atawasogeza hadi katika mgao wa chakula cha serikali lakini kumbe hakuna cha serikali na yeye mwenyewe amebakia hana chakula cha kuikimu familia yake.

"Mimi nashangaa kama serikali kweli itaamua kutowajali watu wa kata yangu ya Hondomairo ambao nao ni wanaKondoa waliokumbwa na tatizo la njaa,au kama serikali inapuuza kwa kudhani kuwa ni mzaha,basi ngoja watu wafe na atakayejibu sijui ni nani,"amesisitiza.

Kata hiyo ya Hondomairo na vijiji vya Mwembeni chenye watu 3494,Hondomairo watu 2896,na Mtiryangwi watu 3696 jumla ni watu 10,086 na kaya ni 2224 ambazo licha ya ukosefu wa chakula lakini pia lipo tatizo kubwa la maji kwa wananchi kutembea umbali mrefu kutafuta maji.

Diwani Kirangi ameiomba serikali kufanya haraka kwani bila kuwanusuru wananchi hao kwa chakula cha msaada hakuna lolote litakalofanyika la maendeleo na wananchi hata mazao waliyolima mashambani mwao hawataweza kuyahudumia ipasavyo hivyo kupata hasara ya nguvu zao,mbegu na fedha za kulimia.
MWISHO.

No comments:

Post a Comment