Mratibu
Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa UNDP nchini Tanzania Dk.
Alberic Kacou akizungumza kwa niaba ya UNDP kuhusiana na kuzinduliwa kwa
Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012 ambapo amesema huu sasa ni wakati
kwa nchi za Afrika haswa zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara kujenga
mazingira ya kuelekea mustakabali wenye uhakika wa chakula.
Mshauri
wa Uchumi UNDP Bw.Amarakoon Bandara akifanya 'presentation' ya Ripoti
hiyo. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dk. Alberic
Kacou, Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Mbene na Mkurugenzi wa UNDP
Tanzania Bw. Phillipe Poinsot.
Mgeni
rasmi Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Mbene na Mratibu Mkazi wa Umoja
wa Mataifa Tanzania, Dk. Alberic Kacou (kulia) wakifuatilia maoni ya
Uchambuzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012 kutoka kwa Maprofesa wa
Vyuo vikuu nchini.
Dr.
John Mduma akifanya majumuisho ya nini kifanyike kukabiliana matatizo
ya uhaba wa chakula yanayolikabili bara la Afrika na Afrika Mashariki.
Profesa Joyce Kinabo wa Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine akieleza uhifadhi wa Chakula kwa ajili ya matumizi ya baadae
Baadhi ya Maofisa wa Umoja wa Mataifa na Wadau wa Serikali wakichangia maoni yao kuhusiana na Ripoti hiyo.
Mgeni
rasmi Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Membe (MB) akisoma hotuba wakati
wa hafla ya Uzinduzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012. Kushoto ni
Mkurugenzi wa UNDP Tanzania Bw. Phillipe Poinsot.
Mgeni
rasmi Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Mbene (MB) akikata utepe kuzindua
rasmi Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa
Umoja wa Mataifa nchini Dk. Alberic Kacou.
No comments:
Post a Comment