TANGAZO ISERESPORTS COLLECTION

TANGAZO SHIWATA

Friday, 20 May 2011

Tamasha la Bob Marley Kigamboni

Na Mwandishi Wetu

JUMUIYA ya watu walio katika  imani za Kirastafarian nchini,TARAMO kimeandaa tamasha  maalum la kukumbuka siku  kuzikwa kwa  mwasisi wa  mindoko ya muziki wa Raggae Ulimwenguni,Nesta Robert Marley, maarufu kama 'Bob Marley'  lililopangwa kufanyika Jumamosi ya Mei 21 mwaka huu katika ufukwe wa Hunter's, Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Hayati Bob Marley alifariki dunia Mei 11, mwaka 1981 na kuzikwa Mei 21 ya mwaka huo nchini Jamaica, ambapo chanzo cha kifo chake kilitokana na ugonjwa wa kansa ya kidole gumba cha mguu iliyosambaa mwilini.

Mwenyekiti wa chama hicho, Ras Bumija alisema jana kuwa tamasha hilo litafanyika kuanzia saa sita mchana na kuendelea mpaka usiku wa manane na kusindikizwa na burudani mbalimbali za muziki wa reggae utakaopigwa 'laivu' na wanamuziki wa miondoko hiyo nchini.

Alizitaja bendi hizo ni pamoja na Afrikabisa inayoongozwa na mkongwe wa muziki wa reggae nchini Jikho Man pamoja na Machifu Band  iliyo chini ya Ras Gwandumi.

Ras Bumija  alizitaja burudani zingine zitakazosindikiza tamasha  hilo  zitatumbuizwa na washindi wa mashindano ya  Tuzo  za Kilimanjaro  kwa mwaka 2011, Hard Mad pamoja na Mzungu Kichaa wa BSS.

Alisema,Hard Mad amealikwa ili aweze kuwatumbuiza  washabiki wamuziki wa reggae na  sambamba na kuwashukuru  kwa kumpigia kura zilizomwezesha kunyakuwa  tuzo ya muziki wa Reggae  mwaka 2011.

Aliongeza Ras Bumija kuwa, Mzungu Kichaa ameingizwa katika ratibaya  burudani kutokana na mchango wake katika fani ya muziki wakizazi kipya nchini unaopendwa na marika yote nchini kutokana na ukweli kuwa, onyesho hilo itahudhuriwa na watu wa marikambalimbali.

"Tumepanga kuwashirikisha wasanii wengi kwa ajili ya kuongezamaana ya onyesho lenyewe likalohusisha pia maonyesho na mauzo ya mavazi ya asili ya Afrika na vyakula vya asili ya bara  hili la watu weusi ambapo kiingilio kimeapangwa kuwa  shilingi elfu tatu ili kuweza kuwapa  fursa washabiki wengi wa muziki nchini kuhudhuria" alisema Ras Bumija na kuongeza.

"Tukiwa miongoni mwa wafuasi wa  imani za Kirastafari tuishio Tanzania tumeliingiza tukio la siku ya kuzikwa kwa hayati Bob marley katika  kalenda  ya matukio yetu ya mwaka ambayo huyaazimisha na kuyakumbuka kwa kushiriki mikusanyiko ya shughuli za kijamii pamoja na burudani za kuenzi kazi za mwasisi wa reggae ulimwenguni".

Alitoa wito kwa washabiki wa muziki  na burudani kujitokeza kwa  wingi katika tamasha hilo la  Kigamboni,kwani litatimiza kumbukumbu ya kweli na ya pamoja kwa jamii ya  wakazi wa  jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment