TANGAZO ISERESPORTS COLLECTION

TANGAZO SHIWATA

Monday 6 September 2010

Tendwa awatwanga Chadema K.O

Monday, September 6, 2010

JOHN TENDWA; MKIONA MTU ANALIA MJUE MAMBO SI MAZURI, MKIONA ANACHEKA MJUE MAMBO YAKE POA!!


Msajili wa vyama vya siasa  nchini Bw. John Tendwa amesema hana taarifa yoyote ya kutoa kuhusiana na pingamizi la CHADEMA dhidi ya mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi CCM.

Katika madai ya Chadema ni kuwa Rais  Jakaya Mrisho Kikwete ameongeza mishahara ya wafanyakazi bila kuhusisha Bunge kitu ambacho kinaenda kinyume na sheria ya Gharama ya Uchaguzi.

Bw. Tendwa ambaye ameahidi kutoa taarifa baada ya siku tano hata hivyo leo waandishi wa habari walipokwenda ofisini kwake kwa ajili kujua hatma ya suala hilo alisema leo ana mkutano mwingine na kuhusu pingamizi la CHADEMA tayari ameshavijibu vyama na pia taarifa ipo Tume ya Uchaguzi ya Taifa .

Hivyo akashauri waende kwa vyama husika na kuwauliza "nendeni kwa wahusika mkawaulize mkiona mtu analia basi mjue mambo yake si mazuri lakini mkiona mtu anafurahia basi mjue mambo yake poa" 

No comments:

Post a Comment