TANGAZO ISERESPORTS COLLECTION

TANGAZO SHIWATA

Wednesday 22 September 2010

ZAIN YAPUNGUZA GHARAMA ZA UPIGAJI SIMU 50%


  Kampuni ya simu za mkononi ya Zain, imetangaza punguzo la gharama za simu kwa wateja wake kwenda mitandao mingine kwa asilimia hamsini.
  Kuanzia sasa, wateja wa Zain watapiga simu kwenda mitandao mingine kwa gharama ya sh 3 kwa sekunde siku nzima.
  Punguzo hili ni muendelezo wa mkakati wa Zain wa kutoza viwango nafuu baada ya kuanzisha sh 1 miezi michache iliyopita.
  Akizungumza na waandishi wa habari Dar-es-salaam leo, Sam Elangalloor, Mkurugenzi Mtendaji wa Zain Tanzania amesema, “Tunajivunia zaidi kwa kuwa mtandao nafuu hapa nchini kuliko mtandao mwingine wowote na katika kuthibitisha hilo, leo tena tumeweza kushusha gharama mpaka nusu ya gharama za mwanzo.
  Tunaamini kila mtanzania ana haki ya kuwasiliana na zaidi ya wateja wetu milioni 5 watafurahia punguzo hili la asilimia 50. Zaidi ya hayo, wateja wa Zain wataweza kupata sms 4 za bure kwenda mitandao mingine yeyote.
  “Wateja wote wa malipo ya kabla na baada watanufaika na punguzo hili. Pia mtakumbuka ya kwamba ni hivi karibuni tu pia tulitoa punguzo za gharama za intanet na za modem hivyo kuwezesha watu wengi zaidi kuwasiliana bila upinzani”, aliongeza Elangalloor.





Muganyizi Mutta


Meneja wa Mawasiliano ya Umma wa Zain Tanzania


0786 670 711

No comments:

Post a Comment