Na Mwandishi Wetu
BENDI
saba za muziki wa dansi zimethibitisha kushiriki mashindano ya Mtandao
wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) na timu nane za soka za maveterani nazo
kumekubali kumtafuta bingwa wa mchezo huo.
Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib alisema jana kuwa
mashindano hayo ambayo yanashirikisha michezo jingine ya mpira wa
kikapu,Sarakasi,kun-fu na kaswida,mshindi wa kila mchezo atakabidhiwa
zawadi katika kijiji cha wasanii Mwanzega Mkuranga kwenye sherehe za
kugawa nyumba Desemba mwaka huu.
Taalib alisema mashindano ya soka yatafanyika Desemba 9
mwaka huu kwenye viwanja cha shule ya Msingi Kitunda zikipambana timu za
Kisarawe veterani, Stakishari veterani, Vituka veterani, Mbagala
veterani, Kigogo TZF, TBC veteran na wenyeji Kitunda na Kivule veteran.
Alisema katika muziki wa dansi bendi zilizothibitisha
kushiriki ni Tanzania One Theatre (TOT), Magereza Jazz (Mkote Ngoma),
Mwenge Jazz (Panselepa),
Hisia Sound (Abdul Salvador) JKT Kimbunga Stereo,Vijana Jazz na Wazee
Sugu ya King Kikii ambazo zitaoneshana umahiri wao kwenye kuimba na
kupiga vyombo.
"Mpaka sasa mashindano ya Kikapu yanayoshirikisha timu 16
za wanaume na nne za wanawake yanaendelea viwanja vya ndani vya
taifa.Timu hizo ni Kurasini Meat, Yellow Jackets, Chui, Kijichi
Worriors, Segerea BC, Jogoo, TMK Rockets, Oilers, Hopper, TM Rockets,
Chang'ombe, Montfort,
"Timu za wanawake ni Ukonga Queens,Vijana Queens,Ukonga
Princesses na Oilers Princesses ambazo bingwa atazawadiwa kikombe na
kukabidhiwa Kiwanja cha kujenga ofisi ya timu"alisema Taalib.
Alisema katika mashindano ya kun-fu klabu zilizothibitisha
kushiriki ni Begeja wu --shu, Karakata Wu-shu na Kigogo Wu-shu ambazo
zitapambana kwenye ujumbe as CCM Mchikichini kwa mchezaji mmoja mmoja.
Naye msimamizi wa mchezo as sarakasi,Selemani Pembe
alisema maandalizi ya mashindano ya mchezo huo yamekamilika na
itavukutanisha vikundi vya Butterfly Arts Group,Happy Center acrobatic,
Black Lion na Jivunie.
Mwisho
No comments:
Post a Comment