SHABIKI wa Klabu ya Yanga, Sudi Kassim Sudi maarufu kwa jina la Big Respect amechukua fomu za kugombea udiwani wa Kata ya Tabata.
Sudi
aliyesindikizwa na familia yake kuchukua fomu hizo aliahidi kuwainua
vijana katika michezo kuongeza ajira kwani anaamini katika kata hiyo
wapo wachezaji wengi wenye vipaji na uwezo wa kucheza mpira Tanzania na
nje ya nchi kama wataendelezwa.
Alisema amekuwa
shabiki na mpenzi wa michezo nchini na katika kata hiyo kwa muda mrefu
hivyo alipoamua kuchukua fomu akipata nafasi hiyo atakuwa kiongozi wa
jamii hasa vijana wa Kata hiyo kwenye michezo kwa kugawa vifaa vya
michezo na kuwakwamua kimaisha.
Alisema sababu
nyingine iliyochangia kuchukua fomu za udiwani ni kutaka kushirikiana na
wakazi wa eneo hilo kuondoa kero zinazoendelea kuwatesaza miundombinu
na maji safi na bora.
Alisema baada ya CCM kumteua Dkt. John Magufuli kuwa mgombea urais ni moja ya sababu iliyochangia kuwa na ari ya kuchukuafomu kwani ana imani naye kuwa ni mchapakazi.
Alisema baada ya CCM kumteua Dkt. John Magufuli kuwa mgombea urais ni moja ya sababu iliyochangia kuwa na ari ya kuchukuafomu kwani ana imani naye kuwa ni mchapakazi.
Awali
Katibu wa CCM kata ya Tabata, Ibrahim Mjanakheri aliyekabidhi fomu hizo
alisema kutoka CCM imteue Dkt. Magufuli kuwa mgombea wao wa Urais hata
wapinzani wameshikwa na kigugumizi cha kuwasimamisha wagombea mwaka huu.
Alisema
Dkt. Magufuli ameongeza ari kwa wanaccm wanaochukua fomu wakiamini kuwa
chama hicho kimerjipanga kuhakikisha kinapata ushindi wa kishindo.
mwisho
No comments:
Post a Comment