TANGAZO ISERESPORTS COLLECTION

TANGAZO SHIWATA

Thursday, 4 June 2015

Kureshy Ufunguoarejea uwanjani

Na Mwandishi Wetu

MCHEZAJI wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Simba, Kajumulo na Mirambo ya Tabora, Kureshy Ufunguo ameamua kurudi uwanjani safari hii kuanzia Soka ya Watoto (Academy) ili kusaka vipaji vya wachezaji wa kuunda Stars baadaye.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Kureshy ambaye aliwahi kuchezea Stars kwa nyakati tofauti alisema anasikia uchungu kuona timu ya Taifa inafanya vibaya mara kwa mara wakati kuna watoto wengi wenye vipaji ambavyo vikiliendelezwa vitaibua wachezaji wazuri.

Alisema amefanya mazungumzo na baadhiu ya maduka ya kuuza vifaa vya michezo likiwemo Isere Sports na kuchagua vifaa ambavyo ataanzia katika kufundisha watoto hao.

Kureshy alisema kwa kuanzia atakuwa anawakusanya watoto katika Klabu aliyoianzisha Kitunda, Kivule ambapo ataanza kuwafundisha kwa nadharia yaani darasani na baadaye uwanjani ambako atatumia uwanja wa Shule ya Sekondari, Misitu, Kivule Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Masoko wa Isere Sports, Abbas Ally alisema Kampuni yake itasaidia kutoa vifaa vya kuanzia mazoezi kama vikinga ugoko (shin guard), mipira na jezi za mazoezi.

Alisema Kampuni itaendelea kutoa misaada kwa mchezaji huyo kwani ni wachache wenye ndoto ya kufufua soka ya Tanzania ambayo kwa sasa Stars haifanyi vizuri katika mashindano mbalimbali ya kimataifa.


Mwisho

No comments:

Post a Comment