TANGAZO ISERESPORTS COLLECTION

TANGAZO SHIWATA

Tuesday 28 April 2015

safari ya wasanii kuhamia Mkuranga imeiva

Na Peter Mwenda

KIKUNDI cha Wasanii 50 wa Mtandao wa Wasanii Tanzania (SHIWATA) wanatarajiwa kuondoka Mei 10, mwaka huu kwenda kuanza maisha mapya ya kijijini ya kulima, kufuga na kuandaa filamu.

Akizungumza katika mkutano wa wanachama uliofanyika mwishoni mwa wiki Dar es Salaam, Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib alisema maandalizi ya wasanii hao kuhamia kijijini yamekamilika  na akiwemo yeye ataongoza msafara huo.

Alisema kati ya wasanii watakaohamia kijijini ni mchezaji wa zamani wa Simba, Dua Said na mwigizaji wa Bongo Movie, Lumola Matovola 'Big' na wengine.

Taalib alisema wasanii wengine katika kikosi chao wapo wapiga picha, walimu wa kutunga hadithi na wasanii watakaocheza filamu na tamthilia hizo.

Alisema wasanii hao pia watagaiwa mashamba ya kulima bustani za mboga mboga, matikiti maji, pilipili na kufuga kuku, bata na mbuzi.

Katika mkutano huo ulihudhuriwa na wanachama zaidi ya 200 ilitolewa ofa ya kuingia wanachama katika kusherekea miaka 10 ya SHIWATA ambayo kilele chake kinafanyika Juni mwaka huu ambako nyumba 30 zitagaiwa.Kijiji cha Wasanii Mkuranga mpaka sasa kimejengwa nyumba 134.

Wanachama hao pia waliwataka wenzao zaidi ya 8,000 kupiga ndiyo za kwenye kura ya maoni ya katiba mpya kwa vile imelenga kuwakomboa wasanii kutoka kwenye wimbi la umasikini.

Mkutano huo pia ulipitisha adhabu ya kuwafukuza wanachama ambao watakwenda kinyume na utaratibu wa uliowekwa wakati wa kujiunga uanachama, usimamizi wa mashamba na kukiukwa kwa sheria za kijiji cha wasanii Mwanzega, Mkuranga.

mwisho

No comments:

Post a Comment