TANGAZO ISERESPORTS COLLECTION

TANGAZO SHIWATA

Thursday 8 May 2014

Mvua zazuia wanafunzi Kivule sekondari kufika shule

Na Peter Mwenda
MVUA za Masika zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam zimewafanya baadhi ya wazazi kuwazuia watoto wao kwenda shule kuhofia kuzama kwenye madaraja yaliyozolewa kulikosababisha magari kushindwa kupita.

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Abuu Jumaa ya Kivule DAr es Salaam , Floida Nkya akizungumza jana alisema kutoka mvua zianze mahudhurio katika shule yake imekuwa hafifu aliwahoji kujua tatizo aliambiwa wazazi wao hawako tayari kuwaruhusu watoto wao kupoteza maisha kwa kuzama maji baada ya madaraja kubomoka.
Alisema shule hiyo yenye wanafunzi 813 kutoka kidato cha kwanza hadi nne kwa sasa wanafunzi wanaohudhuria shule hawafiki 600 hivyo zaidi ya 200 wamekaa majumbani kutokana na hali ya mvua zinazoendelea kunyesha na kusababisha mafuriko katika madaraja.
Mwl. Nkya alisema daraja kubwa lililokuwa linategemewa na wanafunzi waoishi maeneo ya Kitunda, Banana, Ukonga na maeneo mengine ya Jiji la Mto Mzinga daladala hazipiti kwa sababu baada ya kuzolewa na mvua.

Mmoja wa wazazi wa wanafunzi wanaosoma shule hiyo, John Roko alisema wanafunzi wanaosoma shule ya Abuu Jumaa,Shule ya Sekondari Kivule na Shule ya Msingi KIvule hawafiki shuleni kutokana na kuharibika kwa barabara kunakosababisha usafiri kuwa mgumu kwa sababu mabasi ya abiria hayaendi njia hiyo.
Bw. Roko aliomba Serikali kufanya jitihada za haraka kunusuru hali ngumu ya usafiri katika baadhi ya maeneo ya Kata ya Kivule ambayo hayafikiki kabisa kutokana navivuko kuzolewa na mvua na kuwatenganisha wananchi wa sehemu moja hadi nyingine.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kivule, Joseph Gassaya alipoulizwa kuhusu hali hiyo alisema jitihada zinafanyika za kukarabati madaraja na vivuko vilivyozolewa na maji na pia kwa nguvu za wananchi wamejitahidi kujenga madaraja ya muda ili ianze kupitika wakati inasuburi Manispaa ya Ilala na Serikali Kuu kunusuru hali hiyo.
mwisho

No comments:

Post a Comment