TANGAZO ISERESPORTS COLLECTION

TANGAZO SHIWATA

Sunday, 16 September 2012

SUMA LEE: SKENDO INA UJUMBE KWA KINADADA WA KILEO




Na Elizabeth John

BAADA ya kutamba na ngoma yake inayokwenda kwa jina la ‘Utanikumbuka’, Mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ismail Seif ‘Suma Lee’ anajipanga kuachia kibao chake kipya kinachokwenda kwa jina la ‘Skendo’.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Suma Lee alisema yupo katika hatua za mwisho za uandaaji wa kazi hiyo ambayo anaamini itakua gumzo mtaani kutokana na ujumbe ambao wimbo huo umebeba.

“Wimbo huu unaujumbe mzito kwa jamii hasa kwa dada zetu wa kisasa ambao wanapenda kuvaa nguo ambazo sio maadili ya watanzania kwa kisingizio kwamba ni utandawazi,” alisema Suma Lee.

Suma Lee alisema anawashukuru mashabiki wake kwa kumpokea vizuri katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya kitu ambacho kinampa nguvu ya kuendelea kufanya kazi na kutoa nyimbo ambazo zinakua na ujumbe kwa jamii.

Mbali na nyimbo hizo Suma Lee alishawahi tamba na vibao vyake kama, Chungwa, Hakunaga na nyinginezo ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya nchini.

No comments:

Post a Comment