TENGA AAGIZA UCHUNGUZI UFANYIKE SAKATA LA YONDANI KUONDOKA KAMBI YA STARS KWENDA KUSAINI MKATABA YANGA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KLABU
ya soka ya Simba imepokea kwa furaha taarifa kwamba Rais wa Shirikisho
la Mpira was Miguu Tanzania (TFF), Leodger Chila Tenga, ameagiza
kufanyika kwa uchunguzi kuhusiana na namna mchezaji wa Simba na Taifa
Stars, Kelvin Patrick Yondani, alivyoondoka kambini usiku wa kuamkia
Juni 7 mwaka huu.
Katika
barua ambayo Tenga ameiandikia Simba, ameahidi kwamba uchunguzi
utafanyika katika maeneo makuu mawili. Mosi, iwapo ni kweli Yondani
aliondoka kambini usiku, pili iwapo aliondoka kwa ruhusa maalumu au
alitoroka.
Tenga
ameahidi kwamba kama ikibainika kwamba aliondoka bila ruhusa, basi
hatua zitachukuliwa kwa wote waliohusika chini ya taratibu za maadili
kwa wachezaji (Players Code of Conduct).
Kutokana
na kauli hiyo ya Tenga, uongozi wa Simba umeamua sasa kwamba
hautozungumza lolote kuhusiana na masuala ya Yondani. Tayari timu
imewasilisha vielelezo vyake TFF na kote kwingine ambako suala hilo
linaweza kufika. Kilichobaki sasa ni kusubiri vyombo husika vifanye
kazi yake.
Simba
SC inapenda kuchukua nafasi hii kuwaomba wapenzi na wanachama wake
kutulia na kutobabaishwa na taarifa za wachezaji wake kusajiliwa na
timu nyingine.
Kwa
sasa Simba inaendelea na mikakati yake ya usajili unaokidhi vigezo vya
kimataifa ambao ulisababisha msimu uliopita itwae ubingwa wa Tanzania
na kuifunga YANGA goli 5-0 !
Simba si timu ya maneno mengi kwenye usajili bali ni vitendo.
Tunaomba
wanachama wetu watulie na mara ifikapo tareje 15 Juni mwaka huu, mbivu
na mbichi zote zitajulikana. Siku hiyo, Simba itatangaza wachezaji wake
wote iliyowasajili na iliyowaacha.
Simba
ndiyo mabingwa wa Tanzania na washabiki wake wanatakiwa kutembea vifua
mbele popote pale walipo na wasichanganywe na taarifa za pembeni.
Uongozi wa Simba uko makini na unafanya kazi zake kisayansi.
Imetolewa na
Ezekiel Kamwaga
Ofisa Habari
Simba SC
KUELEKEA MCHEZO WA GAMBIA KESHO-POULSEN ALIA NA TFF
TIMU ya soka ya Taifa ‘Kili Taifa Stars’ kesho inashuka katika
dimba la Taifa jijini Dar es Salam kukwaana na Gambia ‘The Scorpions’ katika
mchezo wa mchujo wa kuwania kucheza fainali za kombe la dunia 2014
zitakazopigwa nchini Brazil.
Akizungumza na waandishi wa habari,kocha mkuu wa Stars, Mdenmark Kim Poulsen alisema kikosi kikosi chake kipo katika hali
nzuri ya kimchezo ambao anaamini utakuwa na upinzani mkubwa.
Kocha wa Gambia ,
Mtaliano Luciano Machini akizungumza jana katika mazoezi yao kwenye uwanja wa Karume, alisema itakuwa ngumu kwa sababu wapinzani wao ni
wazuri na wana kasi uwanjani.


No comments:
Post a Comment