Na Mwandishi Wetu
MWANAMUZIKI maarufu wa bendi kongwe ya Msondo ngoma, Muhidin Gurumo aliyelazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ugojwa wa shinikizo la damu anaendelea vizuri.
Akizungumza na Dar es Salaam jana,Msemaji wa bendi hiyo Rajabu MHamila 'Super 'D' alisema afya Gurumo inaendelea vizuri na wakati wowowte anaweza kuruhusiwa kutoka hospitalini hapo.
Alisema kuwa madaktari wanataka kuchukua vipimo vya mwisho kwa kina kujua kila kitu kinachop msumbua katika mwili wake.
"Kwa sasa tunashukuru Mungu afya ya Gurumo inaendelea vizuri tofauti na mara ya kwanza na akiendelea hivi anaweza kuruHUsiwa hivi karibuni"alisema Super D.
Hata hivyo aliwataka wapenzi wa bendi hiyo kumuombea dua mwanamUziki huyo ili apone haraka pia aliongeza kwa kusema maonesho yao ya wiki hii ni kama ifuatavyo, Alhamisi watakuwa Mwandege Mkoa wa Pwani,Ijumaa watapiga katika viwanja vya Leaders Club na Jumamosi watakuwa katika viwanja vya TCC Sigara na Jumapili watamaliza week end katika ukumbi wa Max Bar uliopo Ilala Bungoni.
No comments:
Post a Comment